Saturday, 5 July 2025

Rais Samia Kufanya Ziara Kesho

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku moja nchini Comoro kesho Jumapili tarehe 6 Julai, 2025 kwa mwaliko wa Rais wa Umoja wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Azali Assoumani.

Rais Dkt. Samia atahudhuria Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa nchi hiyo zitakazofanyika katika Uwanja wa Malouzini Omnisport mjini Moroni, ambako anatarajia kuhutubia kwenye sherehe hizo.

Tangu nchi hiyo ipate Uhuru mwaka 1975, Tanzania na Comoro zimeendelea kudumisha uhusiano wa kidugu na wa kihistoria uliojengwa juu ya misingi ya ushirikiano katika nyanja za kiuchumi na kijamii, huku Tanzania ikiendelea kuwa mdau muhimu wa maendeleo ya Taifa hilo.

Ziara ya Rais Dkt. Samia nchini Comoro inadhihirisha dhamira ya dhati ya Tanzania ya kuendeleza ushirikiano wa karibu wa kidugu, kihistoria na kidiplomasia na nchi hiyo pamoja na kuunga mkono juhudi za maendeleo na mshikamano wa nchi hiyo katika miaka 50 ya uhuru wake

Rais Samia Ashiriki Ufunguzi Wa Hema La Arising And Shine Kawe Kwa Mwamposa



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisogeza kitambaa kama ishara ya kuweka jiwe la msingi na kukata utepe Ufunguzi wa Kanisa la Arise and Shine, Kawe Jijini Dar es salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Mtume Boniface Mwamposa mara baada ya kuwasili katika Ufunguzi Kanisa la Arise and Shine, Kawe Jijini Dar es salaam.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia Waumini wa kanisa la Arise and Shine  alipowasili katika hafla ya Ufunguzi wa Kanisa la Arise and Shine, Kawe Jijini Dar es salaam.













Waumini mbalimbali wakati wa Hafla ya Ufunguzi wa Kanisa Arise and Shine ambapo Mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kawe Jijini Dar es salaam

Friday, 4 July 2025

Taarifa Kutoka TFF

Kamati ya Uchaguzi ya TFF Imewang’oa wagombea watano wa nafasi ya Urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kubaki na jina moja la Wallace Karia anayetetea kiti hicho.

Akitangaza ripoti ya usahili wa uchaguzi huo Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF Wakili Kiomoni Kibamba, amesema Karia ndiye mgombea pekee aliyekidhi vigezo na kwa mujibu wa Kanuni na kama kuna mtu anapingamizi bado ana nafasi ya kufanya hivyo .

Kibamba amesema wagombea wengine wanne kati ya sita wamekosa sifa za kukidhi kanuni za uchaguzi huku mgombea mmoja akishindwa kutokea kwenye usahili.

“Kwenye nafasi ya urais kulikuwa na wagombea sita, mmoja hakutokea kwenye usahili na wengine wanne hawakukidhi matakwa ya kikanuni, mgombea mmoja amekidhi matakwa yote ya kikanuni na tumempitisha ambaye ni Wallace Karia,”amesema Kibamba.

Kibamba ameeleza kuwa kwenye nafasi ya wagombea wa nafasi ya ujumbe kulikuwa na wagombea 19 ambapo 17 walihudhuria usahili, saba wamekosa vigezo na kumi wamepitishwa kuendelea na mchakato wa uchaguzi katika hatua inayofuata.

Hata hivyo, Kibamba amesema wagombea ambao wamekosa sifa na kukatwa, wana nafasi ya kwenda kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa ya uchaguzi endapo wataona hawajatendewa haki.

“Sisi ni kamati ya uchaguzi na ni binadamu inawezekana wapo ambao wataona wameonewa wana nafasi ya kwenda kukata rufaa kwenye Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi, wakiturudishia jina lake, sisi hatuna shida, tutalipokea na kuendelea na uchaguzi.

“Kutakuwa na siku sita za kukata rufaa na sisi Kamati ya Uchaguzi tutapokea orodha kamili ya wagombea kutoka kwa Kamati ya rufaa ili tuendelee na hatua inayofuata.

Wagombea sita ambao walichukua fomu ya kugombea urais wa TFF ni Wallace Karia, Richard Shija, Mshindo Msolwa, Ally Mayai, Mustapha Himba na Ally Thabit Mbingo.

Thursday, 3 July 2025

CAF Yatangaza Kanuni Mpya Ligi Ya Mabingwa Africa Na Kombe La Shirikisho

CAF imetangaza kanuni kuu kabla ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho msimu wa 2025/26:

๐Ÿ“Œ Julai 31: Tarehe ya mwisho kwa mashirikisho ya wanachama kuwasilisha vilabu vitakavyoshiriki

๐Ÿ“‹ Vilabu vinaweza kusajili wachezaji hadi 40

๐Ÿ” Substitution 5 kwa kila mechi | Wachezaji 9 benchi

๐Ÿ•’ Wachezaji wapya waliopatikana kwenye dirisha la usajili la Januari lazima wasajiliwe saa 72 kabla ya mechi ili waweze kucheza

๐Ÿ‡ฉ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡ด๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡ช๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡ฑ๐Ÿ‡พ๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡ฌ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ๐Ÿ‡ฟ๐Ÿ‡ฆ๐Ÿ‡ธ๐Ÿ‡ฉ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ณ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

Nchi 12 zenye nafasi ya kuingiza vilabu viwili kwa kila mashindano:

Aljeria, Angola, Cรดte d’Ivoire, Misri, Libya, Morocco, Nigeria, DR Congo, Afrika Kusini, Sudan, Tunisia, na Tanzania.