Monday, 21 January 2019

Simba yaleta wawili wa kimataifa

Uongozi wa Simba umeshusha wachezaji wawili wa Kimataifa ambapo wameanza majaribio leo kabla ya kufikia makubaliano ya kuwasajili

Wachezaji hao mmoja ni mlinzi wa kati na mwingine ni mshambuliaji, wanaweza kuongezwa kwenye kikosi cha Simba kinachoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa

Simba bado ina nafasi za wachezaji wawili ili kukamilisha idadi ya wachezaji 30

Wachezaji hao mmoja ni raia wa Ghana na mwingine ni raia wa Togo

Baada ya ukosoaji mkubwa katika usajili wa Zana Coulibaly ambaye ameshindwa kuonyesha makali, benchi la ufundi la Simba limeamua kuwafanyia makaribio nyota hao kabla ya kuingia nao makubaliano

0 Comments:

Post a Comment