Tuesday 4 July 2023

Rais Samia Aridhia Kufuta Tozo Za Simu

Naibu Waziri wa Wizara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Injinia Kundo Mathew amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la Wizara hiyo chini ya Waziri Nape Moses Nnauye la kufuta tozo katika miamala ya simu.

Naibu Waziri Kundo ameyasema haya leo July 04,2023 akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Rukwa

"Fahari ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Rais ni pamoja na kuwasikiliza Watanzania na Wananchi anaowaongoza, ndio maana ameruhusu na kutoa maelekezo ya moja kwa moja kuondoa tozo katika miamala ya simu"

"Rais wenu kipenzi Mkuu wa Nchi ameruhusu na kutoa maelekezo tozo inayotokana na miamala ya simu iondolewe, hakutokuwa na tozo kwenye miamala ya simu, ile tozo mliokuwa mnasema Rais ameshapangua huyu ndio Mwanamapinduzi halisi wa maendeleo ya Taifa letu"

"Kila Mtu kwenye Familia yake ajue kwamba kuondoka kwa tozo hii ambayo ulitakiwa ukatwe labda Tsh.Elfu 5 haujanunua mboga jamani? ni Rais mmoja tu ambaye ameona uchungu wa Watu wake na sisi tumuunge mkono"

Amesema Naibu Waziri Injinia Kundo

0 Comments:

Post a Comment