Friday 7 July 2023

Simba Yatajwa Kumalizana Na Aubin Kramo Kouamé,

Klabu ya Simba imetajwa kufikia makubaliano ya usajili na Winga hatari wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Aubin Kramo Kouamé.

Baada ya kuinasa saini ya Essomba Onana ambaye anamudu kucheza nafasi zote za winga, ujio wa Kramo unakwenda kuimarisha zaidi eneo hilo la Ushambuliaji.

Winga huyo anatumia miguu yote kwa ufasaha hivyo kumfanya kuwa mchezaji ambaye Simba inaweza kumtumia katika nafasi zote za winga na hata kiungo Mshambuliaji.

Simba yatajwa kumalizana na Aubin Kramo Kouamé,Aubin Kramo Kouamé Simba,Aubin Kramo Kouamé Simba SC, Simba yatajwa kumalizana na Kramo Aubin,Simba yamalizana na Aubin Kramo Kouamé.Ukizungumzia wachezaji waliong’ara katika kikosi cha ASEC Mimosas kilichocheza Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu uliopita wa 2022/2023, hutoacha kumtaja Aubin Kramo Kouamé.

Katika dirisha hili la usajili, Simba imefanya maboresho katika kila eneo kuanzia mlinda lango, safu ya ulinzi, kiungo na safu ya Ushambuliaji.


0 Comments:

Post a Comment