Thursday, 22 April 2021

Azamu Yashikwa shati

Azam Fc imeshindwa kupata ushindi mbele ya Dodoma Jiji ikiambulia sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Jamhuri Dodoma

Ni matokeo ambayo yanawabakisha Azam Fc nafasi ya tatu wakifikisha alama 51 alama sita nyuma ya Yanga ambayo iko kileleni ikiwa na alama 57 na mchezo mmoja mkononi

Yanga itacheza na hao hao Azam Fc siku ya Jumapili katika mchezo utakaopigwa saa mbili na robo usiku uwanja wa Benjamin Mkapa

Katika mchezo mwingine uliopigwa leo, Ihefu Fc wameigaragaza Tanzania Prisons kwa kupata ushindi wa bao 1-0

 

0 Comments:

Post a Comment